• Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • e-Mrejesho |
Manyara Regional Secretariat
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Madini
    • Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Picha
    • Hotuba
    • Video
    • Habari

Manyara jiandaeni na Mashindano ya ngumi Kitaifa-Mkuu wa Mkoa

Imechapishwa Tarehe: August 25th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Joseph Joseph Mkirikiti amewataka wananchi wa Mkoa huo pamoja na mikoa ya jirani kujiandaa na mashindano ya ngumi Kitaifa yanayotarajiwa kuanza kufanyika Septemba 6, 2020 Mkoani humo.

Mheshimiwa Mkirikirti ameyasema hayo jana Agosti 24 alipokuwa akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Motel Papaa Mjini Babati.

“Ngugu wananchi wa Mkoa wa Manyara kuanzia mwezi wa tisa tunatarajia kuwa na mashindano yabondia Kitaifa yatakayofanyika hapa makao makuu ya Mkoa kwa kukutanisha mabondia kutoka mikoa yote ya Tanzania bara, hivyo nawataka mjiandae kupokea ugeni huo na pia muanze kufanya maandalizi mbalimbali kwani ugeni huo utakuwa na fursa mbalimbali katika Mkoa wetu” Alisema Mhe.Mkirikiti.

Katika kujiandaa na mashindano hayo Timu ya Bondia ya Mkoa wa Manyara tayari imeshapatikana kwa kufanya mchujo wa mabondia kutoka wilaya zote tano za Mkoa na ipo kambini tangu Agosti 5,2020 ili kuhakikisha wanachukua ubingwa wa Taifa.

Fursa mbalimbali kama za usafirishaji,Huduma za chakula, malazi,huduma za simu na nyingine nyingi zinaweza kupatikana kutokana na mahindano hayo na hivyo kuwafanya wakazi wa Manyara kujiongezea kipato chao na kwa Taifa kwa ujumla.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Manyara amewataka wananchi kufanya kazi kwa bidi na kuacha kujihusisha na vitendo vya kihalifu kama uvutaji bangi,utumiaji wa madawa ya kulevya, vitendo vya ubakaji na tabia za wizi.

“Pamoja na Mji wetu wa Babati kuachangamka na kuonesha sura ya kuwa Makao Makuu ya Mkoa bado kuna watu wachache wanatuletea sifa mbaya katika Mkoa wetu kwa vitendo vya ajabu ajabu,hivyo nawataka wote wenye vitendo hivyo kuacha mara moja la sivyo hatua kali za kisheria zitafuata kwa kuwafuatilia wote na kuwakamata” Alisisitiza Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara ambaye yupo katika ziara ya kujitambulisha kwa wananchi tangu ateuliwe kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli pia alisikiliza kero mbalimbali kwa wananchi wa Mji wa Mji Babati na kuzitafutia ufumbuzi kwa kuwataka wataalamu wa Halmashauri zote za Mkoa huo kujenga utaratibu wa kutatua kero za wananchi mapema ili kuondoa manung’uniko kwa wananchi.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI - BABATI MJI June 29, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI - BABATI MJI June 17, 2022
  • NAFASI ZA KAZI - HALMASHAURI YA MJI WA BABATI May 24, 2022
  • Kanuni za Utoaji na Usimamizi wa Mikopo Kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana Na Watu Wenye Ulemavu May 17, 2019
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA 39 CHA RCC MKOA WA MANYARA

    February 20, 2025
  • KIKAO CHA BODI YA BARABARA MKOA WA MANYARA

    February 19, 2025
  • RC SENDIGA AZINDUA KLINIKI YA MADAKTARI BINGWA MKOANI MANYARA

    November 20, 2024
  • TIMU YA USIMAMIZI WA AFYA MKOA WA MANYARA WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA DHARURA ZA KIAFYA NA MAJANGA

    November 14, 2024
  • Tazama Zote

Video

Vuta Pumzi, Funguka, Ongea na Mkuu wa Mkoa
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • wizara ya Fedha
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2022 Manyara Region Secretariet . All rights reserved.