• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara (MMM) |
    • Barua pepe za Wafanyakazi |
    • Malalamiko |
Manyara Regional Secretariat

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Sekretarieti ya Mkoa wa Manyara

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Sehemu
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Huduma za Elimu
      • Serikali za mitaa
      • Huduma za Afya
      • Utawala na Rasilimali Watu
    • Vitengo
      • Uhasibu
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • TEHAMA
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Mji wa Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Babati
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hanang'
    • Halmashuri ya Wilaya ya Mbulu
    • Halmashauri ya Mji Mbulu
    • Halmashauri ya wilaya ya Kiteto
    • Halmasahuri ya Wilaya ya Simanjiro
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Kilimo
    • Madini
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Elimu
    • Huduma kwa wateja
    • Huduma kwa wafanyakazi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogondogo
    • Ripoti
    • Mpango Kazi
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Fomu za Kujiunga na Bangdalalu Sekondari
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Habari
  • Blog

Historia

Ndugu Msomaji karibu katika Tovuti rasmi ya Mkoa wa Manyara.Sekretarieti za Mikoa zilianzishwa kwa mujibu wa sheria namba 8(1) cha sheria ya Tawala za Mikoa sura ya 97 sheria ya mwaka 1997. Sekretarieti za Mikoa zimepewa majukumu mbalimbali ya kutekeleza ikiwa ni pamoja na kuratibu utekelezaji wa shughuli za wizara za kisekta,kusimamia utekelezaji wa sera za Kitaifa ndani ya eneo la Mkoa,kufuatilia na kutathimini utoaji na upatikanaji wa huduma katika mikoa, kupitia bajeti za Halmashauri na kutoa ushauri kuhusu sera za Taifa,kufuatilia na kutathimini matumizi ya ruzuku ya Serikali za Mitaa zilizo katika Mikoa.Aidha kwa mujibu wa sheria Na 19 ya 1997 Majukumu ya Sekretarieti ya Mkoa ni kumsaidia Mkuu wa Mkoa kutekeleza majukumu yake, majukumu hayo ni kama vile Ulinzi na usalama, uchumi, utamaduni, maendeleo ya Mkoa, pamoja na kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa shughuli zote zinazotekelezwa katika Serikali za Mitaa pamoja na kutoa mwongozo kwa Sekta binafsi.

Mkoa wa Manyara ulianzishwa kwa tangazo la Serikali Na. 367 lililotolewa tarehe 27 Julai, 2002 na kuchapishwa katika gazeti la Serikali tarehe 2 Agosti, 2002 baada ya kugawanywa kwa Mkoa wa Arusha ambao kabla na wakati wa kipindi cha Uhuru ulijulikana kama Jimbo la Kaskazini (Northern Province). Mkoa wa Arusha ulianza kutumia rasmi jina hilo mwaka 1963.Miongoni mwa Wilaya zilizounda Mkoa huo ni Mbulu na Maasailand ambazo sehemu kubwa iko katika Mkoa wa Manyara sasa. Wilaya hizo ziligawanywa kama ifuatavyo:- Wilaya ya Mbulu ilianzisha Wilaya ya Hanang mwaka 1969 na Hanang ikianzisha Babati mwaka 1985, wakati Wilaya ya Maasailand iligawanywa kwenye Wilaya ya Kiteto mwaka 1974 ambayo pia iligawanywa na kuanzisha Wilaya ya Simanjiro mwaka 1993. Aidha, baada ya kugawanywa kwa Mkoa wa Arusha, Wilaya za Mbulu, Hanang’, Babati, Kiteto na Simanjiro ziliuunda Mkoa wa Manyara.



Mkoa wa Manyara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 27000.Mkoa wa Manyara unapakana na Mikoa ya Singida na Shinyanga upande wa magharibi, Mkoa wa Dodoma upande wa kusini, Mkoa wa Tanga upande wa mashariki na Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro Upande wa kaskazini.

Makao makuu ya mkoa wa Manyara yapo Babati Mjini.

Idadi ya watu, Mkoa wa Manyara una jumla ya wakazi 1,425,131 kati ya hao Wanaume ni 717,085 na Wanawake ni 708,046 (sensa ya mwaka 2002) Idadi hiyo imepatikana katika wilaya zifuatazo (idadi ya wakazi katika mabano mwaka 2002): Babati (303,013), Hanang (205,133), Mbulu (237,882), Simanjiro (141,676) na Kiteto (152,757).

Sensa zinaonyesha kwamba ni kati ya mikoa ya Tanzania yenye ongezeko kubwa la wakazi. Pia ni kati ya mikoa yenye maambukizi machache zaidi ya Ukimwi.

Makabila Makuu katika Mkoa



WAKAZI WA WILAYA
KUNDI KUU
KUNDI DOGO
BABATI
Wabantu
Wambungwe,Warangi,Wachagga, Wapare, Wangoni,Waasi na Makabila mengine
Nilo Hamites
Wagorowa, Wa-Iraqw, Maasai, Barbaig
HANANG’
Wabantu
Wanyiramba, Warangi, Wanyaturu na makabila mengine
Nilo Hamites
Wabarbaig, Wa-Iraqw.
MBULU
Nilo Hamites
Wa-Iragw, Wabarbaig, Wahadzabe.
KITETO
Wabantu
Wagogo, Warangi, Wanguu, Wakaguru, Wasambaa na makabila mengine
Nilo Hamites
Wamaasai, Waburunge, Wa-Akea (Wandorobo)
SIMANJIRO
Wabantu
Wanguu, Wachagga, Wapare, Warangi na makabila mengine.
Nilo Hamites
Wamaasai na Wandorobo[ Wa-Akea ]


NB: Kwa sasa kuna makabila mengine madogo madogo. Aidha makabila ya Hadzabe na Akea yanahitaji uangalizi kwa vile huishi kwa kutegemea uwindaji, mizizi, matunda na kula asali.

HALI YA HEWA YA MKOA

Mkoa unapata wastani wa Mvua kati ya mm 450 na mm1200 kwa mwaka. Kuna misimu miwili ya mvua. Mvua za muda mfupi ambazo hunyesha kati ya Oktoba na Desemba katika baadhi ya maeneo ya Wilaya za Kiteto, Hanang’, Babati na Mbulu. Mvua za muda mrefu hunyesha kati ya mwezi Februari na Juni. Hali ya hewa ni nyuzi joto 130C wakati wa masika na nyuzi 330C wakati wa kiangazi kutegemeana na msimu na mwinuko wa ardhi. Mkoa upo katika mwinuko kati ya mita 1000 – 2000 juu ya usawa wa bahari

WABUNGE WA WA MKOA WA MANYARA.
Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2020 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi 7 yafuatayo:

  • Babati Mjini : Pauline Philipo Gekul (CCM)
  • Babati Vijijini : Daniel Baran Silo (CCM)
  • Hanang’ : Mhandisi Samwel Hayuma Xaday (CCM)
  • Kiteto : Edward Ole Lekaita Kisau (CCM)
  • Mbulu Mjini : Paulo Zacharia Issay (CCM)
  • Mbulu Vijijini : Flatei Gregory Massay (CCM)
  • Simanjiro : Christopher Olonyokie Ole Sendeka (CCM)


  •   Pia Mkoa wa Manyara una wabunge watatu wa Viti Maalum ambao ni
    • Rejina Ndege Qwaray-(CCM) (kupitia umoja wa wazazi)
    • Martha J. Umbula- (CCM)  (kupitia umoja wa wazazi)
    • Asia Abdulkarim Hamlaga- (CCM) (kupitia umoja wa Vijana)

Wakuu wa Mkoa walioongoza Mkoa wa Manyara toka 2002 hadi sasa.

Na

Jina Kamili

Mwaka alionza
Mwaka alioondoka
1.
Mhe.Kanali (mst) ANATOLI A. TARIMO
22/08/2002
10/05/2007
2.
Mhe. HENRY D. SHEKIFU
10/05/2007
19/08/2010
3.
Mhe.ELASTON J. MBWILO
19/09/2011
06/12/2014
4.
Mhe.Dkt. JOEL N. BENDERA
06/12/2014
26/10/2017
5.

6.
Mhe.ALEXANDER P. MNYETI

Mhe.JOSEPH JOSEPH  MKIRIKITI
26/10/2017

16/07/2020
15/07/2020

Mpaka sasa


Makatibu Tawala Walioongoza Mkoa wa Manyara toka 2002 hadi sasa

Na.

Jina Kamili

Mwaka alioanza
Mwaka alioondoka
1.
PHINIAS L. NNKO
22/08/2002
04/12/2007
2.
THOMAS G. SOWANI
24/09/2008
07/07/2010
3.
BITEGEKO B. CLAUDIO
08/07/2010
15/04/2013
4.
Mhandisi. OMAR A. CHAMBO
03/02/2014
23/10/2015
5.

6.
ELIAKIM C. MASWI

MISSAILE  R. MUSA
23/10/2015

28/07/2018
27/07/2018

Mpaka Sasa







Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MKOA WA MANYARA December 18, 2020
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI JIMBO LA BABATI MJINI October 21, 2020
  • MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2018 MKOA WA MANYARA December 27, 2017
  • OR-TAMISEMI YATANGAZA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA MSINGI NA SEKONDARI JULAI 2018 July 17, 2018
  • Tazama Zote

Habari mpya

  • Vijana Kiteto wanufaika na Mikopo ya Halmashauri

    January 05, 2021
  • Babati watakiwa kuchangamkia Mikopo ya Serikali

    January 04, 2021
  • Waziri wa Kilimo awataka Wakulima wa ngano kuongeza uzalishaji

    December 24, 2020
  • Njooni muwekeze Manyara- RC Manyara

    December 22, 2020
  • Tazama Zote

Video

Nangwa Sekondari katika muonekano mpya
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Miongozo ya OR-TAMISEMI
  • Kanuni za Uchaguzi
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi
  • Mwongozo wa OPRAS
  • Maadili
  • Fomu za Opras
  • Fomu ya Ugonjwa

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya TAMISEMI
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Waliotembelea

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Barabara ya Babati - Singida

    Anuani ya Posta: P.O.BOX 310

    Simu ya mezani: 027-2510066

    Simu ya kiganjani:

    Barua pepe: rasmanyara.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Siri
    • Kanusho
    • Ramani Elekezi

Copyright ©2020 Manyara Region . All rights reserved.